Uasi wa pili ulifuata haraka tarehe 29 Julai 1966 na safari hii kikundi cha maafisa kutoka kaskazini walimwua Ironsi na kuchukua serikali mkononi mwao chini ya uongozi wa jenerali Yakubu Gowon. Mwaka uliofuata 1967 serikali mpya ilianza kubadilisha muundo wa utawala; mikoa mitatu ya Nigeria iligawiwa kuwa majimbo 12. Waigbo walisikitika ya kwamba mipaka ilichorwa kwa kusidi la kuacha maeneo ya Delta penye mafuta ya petroli nje ya majimbo penye Waigbo wengi. Ili ilitazamiwa kama jaribio la kuwatenga Waigbo na malighafi hizi.
MENU
Saturday, September 17, 2016
IFAHAMU BIAFRA YA NIGERIA
Labels:
HISTORIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment